Jumanne, 24 Shawwal 1446 | 2025/04/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hotuba Inayohusu Bendera za Rayah na Liwaa za Mtume (saw) Ilipambwa kwa Takbira na Machozi katika Soko Kuu la Port Sudan

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba yake ya kisiasa ya kila wiki, iliyokuwa na kichwa: “Je, Mtume (saw) alikuwa na bendera na Rayah?”, mnamo Jumatatu tarehe 28 Jumada al-Akhirah 1446 H sawia na 30/12/2024 M. Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alizungumza akisisitiza kuwa bendera ya Liwaa na Rayah katika Uislamu ni suala la dini, itikadi, mfumo na nembo ya Uislamu. Mtume (saw), ana benera (Liwaa) nyeupe kama bendera ya amiri jeshi, na bendera (Rayah) nyeusi kwa makamanda wa majeshi na vikosi, na inaitwa Uqab, zimeandikwa juu yazo “La Ilaha illa Allah Muhammad Rasulullah”.

Soma zaidi...

Ujasiri Wenu Kwa Mwenyezi Mungu, Enyi Madhalimu, Unatangaza Kukaribia Mwisho Wenu

Wakati Mayahudi walipokuwa wakiizingira Hospitali ya Kamal Adwan mjini Gaza, kisha kuivamia, kisha kuichoma moto, na kuwapeleka wagonjwa, majeruhi, na wafanyikazi wa matibabu kwenye hatima isiyojulikana hadi wakati wa kuandika taarifa hii, badala ya mamlaka hiyo kulaani uhalifu wao, badala ya kuuchochea ulimwengu dhidi ya vitendo vyao viovu na vya kikatili, badala ya kuuhamasisha Umma wa Kiislamu kuwanusuru watu wa Gaza, badala ya kuona haya kwa heshima ya majeraha ya Gaza na Ukingo wa Magharibi, walikataa kufanya chochote isipokuwa kuwa Jenin, wakifanya matendo ya Mayahudi na kuwanyanyasa watu wa Palestina mithili Mayahudi wanavyowanyanyasa.

Soma zaidi...

Wito kwa Waislamu kwa Jumla, na kwa Watu wa Ash-Sham Hasa

Enyi Waislamu kwa jumla, na watu wa Ash-Sham hasa: Kiongozi wa Hizb ut Tahrir, asiyewadanganya watu wake, anakuonyeni juu ya mikono ya mashetani wa wanadamu wanaotaka damu yenu imwagike bure, ili msifikie wema msafi na dhahiri, kuhukumu kwa yale yote aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu, bali hukmu iliyotungwa na mwanadamu lakini yenye jina na maana tofauti. Badala ya kuwa Umma ambao makafiri wanauchukulia kwa uzito, mumerudi kuwa wafuasi wa makafiri wakoloni na vibaraka wao, na huu ni uhalifu, Mwenyezi Mungu aepushie mbali, ambao hatima yake ni udhalilifu duniani na adhabu kali kesho Akhera.

Soma zaidi...

Mkutano wa Waandishi Habari juu ya Sarafu na Mshtuko wa Nixon

Kabla ya kuanzishwa kwa sarafu, watu walitumia ubadilishanaji wa bidhaa kwa huduma. Kwa kuwa dhahabu na fedha zimezingatiwa kuwa madini ya thamani yenye kima cha asili kwa binadamu tangu nyakati za zamani, zilitabanniwa kama pesa, huku sarafu zikichongwa kwazo ili kurahisisha ubadilishanaji. Dhahabu, hasa, inajulikana kwa kuhimili kwake kuharibika kwa muda mrefu.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir Inalingania Ukombozi wa Ardhi za Waislamu kutokana na Ukoloni

Hizb ut Tahrir imekuwa mada ya mjadala wa kijamii ndani ya duara zenye ushawishi za Pakistan. Mjadala huo unajumuisha kama tiba za Shariah kwa matatizo ambayo Hizb ut Tahrir inayawasilisha zinapaswa kutekelezwa ili kuepuka matatizo mengi ambayo Pakistan inakabiliana nayo. Kuna mjadala mkali kuhusu Hizb ut Tahrir yenyewe, ikiwemo kupigwa marufuku kwake nchini Pakistan na msimamo mkali dhidi yake katika suala la mateso, unyanyasaji na kifungo. Kwa maslahi ya mjadala wenye tija, mambo yafuatayo ni ya kuzingatiwa na wenye ushawishi kwa jumla na watunga sera, waandishi wa habari, mashirika ya haki za binadamu na ndugu wanasheria hasa.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu