Unafiki wa Kisiasa katika Demokrasia Kamwe Hautaisha Mpaka Tuubadilishe kwa Siasa za Kiislamu
- Imepeperushwa katika Malaysia
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo tarehe 06/01/2025, rufaa ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Najib Tun Razak kuhusu kuwepo kwa amri ya nyongeza ya Mfalme, inayomruhusu kutumikia kifungo chake kilichosalia chini ya kifungo cha nyumbani, imekubaliwa na mahakama kwa wingi wa 2-1. Majaji wa Mahakama ya Rufaa kisha wakaamuru kesi hiyo irudishwe katika Mahakama Kuu ili ombi la Najib la uhakiki wa mahakama lisikizwe na jaji mpya. Amri hii ya nyongeza, ambayo ni sehemu ya mchakato wa msamaha wa kifalme, imekuwa jambo la kawaida, ambalo halijawahi kutokea katika asili yake. Sambamba na hilo, kulikuwa na jambo jengine - mkusanyiko mkubwa wa kuonyesha mshikamano uliokusanyika nje ya mahakama, ulioandaliwa na vyama ambavyo hapo awali vilikuwa wapinzani wa kisiasa wa Waziri Mkuu huyo wa zamani.