Jumatano, 06 Sha'aban 1446 | 2025/02/05
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Katika Kumbukumbu ya Kila Mwaka ya Kuvunjwa Khilafah na ukingoni mwa kuregea kwake, Tunaulingania Umma wa Kiislamu Uharakishe Kuisimamisha

Tangu Khilafah ilipovunjwa mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H, sawia na 3 Machi 1924 M, Ummah umekuwa ukipitia majanga na kushindwa mfululizo; kuanzia mgawanyiko wa ardhi yake, mpaka kunyang'anywa mali yake, na kuwaua wanawe, na kudhihakiwa matukufu yake na mashambulizi dhidi ya Sharia yake. Hata hivyo, leo Khilafah iko karibu zaidi kuliko wakati mwingine wowote kurudi, Rayah (bendera) yake iko tayari kupeperushwa kwa mara nyengine tena juu ya ardhi za Waislamu. Kwa hakika, tunaishi katika wakati unaokumbusha usiku ule watu wa Madina walipokuwa wakishauriana, wakikubaliana kwamba wakati umefika wa kumpa Bay'ah bwana wetu Muhammad (saw) kama kiongozi wao wa kisiasa na mkuu wa dola.

Soma zaidi...

Watawala Vibaraka Wana Hofu juu ya Tishio kwa Viti vyao vya Utawala lakini Hawana Wasiwasi juu ya Vita vya Mauaji ya Halaiki!

Mnamo Jumanne na Jumatano, wizara za mambo ya nje za Jordan, Saudia, Imarati, Mamlaka ya Palestina na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu zililaani uchapishaji wa akaunti rasmi unaohusiana na umbile la Kiyahudi wa ramani za kanda hiyo ambazo ni pamoja na maeneo ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, Jordan, Lebanon na Syria, wakidai kwamba hayo ni ramani ya kihistoria ya umbile la Kiyahudi. Walionyesha wasiwasi wao kuhusu masuala mawili.

Soma zaidi...

“Mayahudi Hawawi Radhi Nawe, Wala Wakristo, Mpaka Ufuate Mila Yao” [Al-Baqarah: 120]

Utawala mpya nchini Syria umetoa taarifa mtawalia kuhusu mfumo wa serikali ambayo wananuia kutekeleza baada ya dhalimu kutoroka. Ni wazi kuwa si mfumo aliouweka Mwenyezi Mungu (swt) bali ni mfumo wa kisekula unaotenganisha dini na maisha kwa kisingizio cha kuwapa watu uhuru wa kuchagua mfumo wa utawala. Wanawaruhusu waandamanaji wa kike wanaodai uhuru na kuvua hijab, huku wakiwateka nyara waandamanaji wasafi wanaodai kuachiliwa kwa jamaa zao wanaotaka kutabikishwa kwa Shariah ya Mwenyezi Mungu (swt)!

Soma zaidi...

Mabadiliko ya Kweli Yanaweza Tu Kuja Kutokana na Mradi Unaotokana na Aqidah ya Ummah. Ni nani Aliye Nao?

Umma wa Kiislamu umeishi kwa karne moja katika unyonge na udhalilishwaji, mfarakano na mgawanyiko, na utegemezi kwa nchi kubwa. Hii inatokana na matendo ya watawala Ruwabidha (wajinga watepetevu) ambao hawaheshimu udugu au ahadi yoyote, wanachojali tu ni kubakia kwenye viti vyao vibovu (vya utawala), kutekeleza mipango ya nchi za Kikafiri katika ardhi zetu ili kukazanisha udhibiti wao juu yetu na kupora mali zetu. Wamesimama dhidi ya kila mtu anayewapinga au kutokubaliana nao, au kujaribu kuwabadilisha, na kuwaweka chini ya kifungo, mateso, mauaji, na ukiukaji wa matukufu. Bashar al-Assad na utawala wake wa kihalifu sio wa mwisho wao, ambaye uhalifu dhidi ya watu wake ulifichuliwa na matukio ya hivi majuzi nchini Syria, uhalifu ambao ni wa aibu na kuwafukuza wale wenye maumbile yaliyo sawa.

Soma zaidi...

Matukio ya Uhalifu Yanayofichuliwa Katika Magereza ya Dhalimu wa Ash-Sham Yanapasa Kuwasha Moto Nyoyoni mwa Wana wa Ummah Kuwateketeza Watawala

Katika siku chache zilizopita baada ya kutoroka kwa dhalimu Bashar na kuanguka kwa utawala wake muovu, matukio ya uchungu na makali yalifichuliwa ambayo yalivunja nyoyo za Waislamu. Kwani waliona kwa macho yao ukubwa wa jinai na ukatili ambao utawala wake uliamiliana nao kwa ndugu na dada zao katika vituo vya uzuizi na magereza: kuanzia na kuwekwa kwao kizuizini kwa miongo kadhaa katika magereza ambayo yalikosa mahitaji msingi zaidi ya kibinadamu, kisha njaa, ukandamizaji na mateso ya kikatili ambayo magereza hayo na kuta zinayazungumzia, na seli, nguzo na zana za mateso zinazosimulia hadithi zao, na miili ya wahasiriwa waliopatikana wamekufa na kukatwakatwa inamfichua.

Soma zaidi...

Marekani Yaogopa Kuangamia kwa Tawala za Vibaraka katika Nchi za Waislamu na Kuibuka kwa Khilafah

Marekani haiachi kuonyesha hofu yake ya kuangamia kwa tawala vibaraka katika nchi za Waislamu mara kwa mara. Hofu hii inaonekana kwenye ndimi za viongozi wake; Mshauri wake wa Usalama wa Kitaifa Jake Sullivan anathibitisha kwamba itafanya kazi kuimarisha Jordan, umbile la Kiyahudi (Kizayuni), na Iraq ili mzozo wa Syria usihamia kwao. Siku chache zilizopita, Waziri wake wa Mambo ya Nje Antony Blinken alisisitiza katika hotuba yake kabla ya Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa NATO juu ya ulazima wa kuzuia kuregea kwa Dola ya Khilafah.

Soma zaidi...

Hongera Ash-Sham na Watu wake kwa Kumpindua Mtawala dhalimu na Utawala wake, Sasa ni Mbele Kuelekea Khilafah Rashida

Asubuhi ya leo, Jumapili tarehe 8/12/2024 M, na katika siku ya 12 ya operesheni ya “Kuzuia Uvamizi”, wapiganaji waliweza kuingia katika mji mkuu wa Syria, Damascus, na kupindua utawala wa Bashar al-Assad, ambaye Reuters iliripoti - ikiwanukuu maafisa wa Syria – kwamba aliuacha mji mkuu na kuelekea kusikojulikana. Hivyo, wapiganaji wa upinzani waliweza kuikomboa Idlib, Aleppo, Hama, Homs na Damascus, na kuwaachilia maelfu ya wafungwa waliokuwa wakizuiliwa na utawala wa kihalifu katika vyumba vya chini vya jela zake ovu kwa miaka na miongo kadhaa.

Soma zaidi...

Watawala wa Bara Arabu Wanashindana katika Ufisadi na Utiifu kwa Maadui wa Ummah!

Siku chache zilizopita, watawala wa Imarati walijigamba juu ya uhamasishaji wao mkubwa wa kuwafikia wauaji wa Rabbi wa Kiyahudi, Zvi Kogan, kwenye ardhi zao, na kupongeza umakini wa vyombo vya usalama na kasi ya taratibu zao zilizochangia kufichua tukio hilo, baada ya huduma hizi zote kufanya kwa muda wote, kulingana na yale yaliyoelezwa katika taarifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani. Wakati huo huo, Imarati na Wizara yake ya Ulinzi haikujitolea kuwanusuru zaidi ya mashahidi elfu 44 na elfu 104 waliojeruhiwa huko Gaza, ingawa muuaji wao anajulikana na haihitaji uchunguzi au umakini wa vyombo vya usalama kumfikia.

Soma zaidi...

Maamuzi ya Mkutano wa GCC ni Ushirikiano katika Dhambi na Udanganyifu

Mnamo Jumapili, tarehe 1 Disemba 2024, katika taarifa ya mwisho iliyotolewa na kikao cha 45 cha Baraza Kuu la Baraza la Ushirikiano wa Ghuba iliyoandaliwa na Serikali ya Kuwait, viongozi wa nchi za Baraza la Ushirikiano wa Ghuba (GCC) na wawakilishi wao walitoa wito wa kumalizwa kwa uhalifu wa mauaji na adhabu ya pamoja huko Gaza, uhamishaji wa wakaazi, uharibifu wa vifaa na miundombinu ya raia. Walitoa wito wa kuingilia kati kulinda raia, kusitisha vita, na kufadhili mazungumzo mazito ili kufikia suluhu endelevu, wakisisitiza misimamo yao madhubuti kuhusu kadhia ya Palestina, kukomesha uvamizi huo, na uungaji mkono wao kwa uhuru wa watu wa Palestina juu ya ardhi zote za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu tangu Juni 1967, na kuanzishwa kwa dola huru ya Palestina na Jerusalem Mashariki kama mji mkuu wake, na kuhakikisha haki za wakimbizi, kwa mujibu wa Mpango wa Amani wa Kiarabu na maazimio ya uhalali wa kimataifa. Kuhusiana na Lebanon, viongozi hao walithibitisha mshikamano kamili na Lebanon.

Soma zaidi...

Watawala wa Iran ni Uhalisia tu wa Sauti na Maonyesho ya Fataki Hawana Uhusiano Wowote na Ushindi au Ukombozi

Kamanda wa Walinzi wa Mapinduzi ya Iran, Meja Jenerali Hossein Salami, alithibitisha katika ufunguzi wa mazoezi ya mapambano ya usalama ya “Nasrallah” kwamba “umbile la Kizayuni linakosea ikiwa linadhani kuwa Hizbullah itatoka nje ya uwanja kwa kuwauwa viongozi wake,” na kubainisha kuwa “chama hicho ni vuguvugu kubwa ambalo haliwezi kuzimwa wala kumalizwa.” Akalitisha umbile la Kiyahudi kwa kusema: “Leo tuna nyinyi machoni mwetu, na tutapigana mpaka mwisho, na hatutakuruhusuni kudhibiti hatma ya Waislamu, na tutalipiza kisasi, nanyi mtapata pigo chungu, na lazima musubiri.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu