Enyi Waislamu kwa jumla, na watu wa Ash-Sham hasa: Kiongozi wa Hizb ut Tahrir, asiyewadanganya watu wake, anakuonyeni juu ya mikono ya mashetani wa wanadamu wanaotaka damu yenu imwagike bure, ili msifikie wema msafi na dhahiri, kuhukumu kwa yale yote aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu, bali hukmu iliyotungwa na mwanadamu lakini yenye jina na maana tofauti. Badala ya kuwa Umma ambao makafiri wanauchukulia kwa uzito, mumerudi kuwa wafuasi wa makafiri wakoloni na vibaraka wao, na huu ni uhalifu, Mwenyezi Mungu aepushie mbali, ambao hatima yake ni udhalilifu duniani na adhabu kali kesho Akhera.